soma mbinu zitakazo kuwezesha kufaulu mitihani na namna ya usomaji mzuri utakao kusaidia kufauru mitihani yako. au kumwezesha mwanafunzi wako au mtoto wako.
1. Big result now ufaulu mkubwa sasa Big result now ufaulu mkubwa sasa Big result now ufaulu mkubwa sasa
MBINU ZA
KUFAULU
MITIHANI
Mimi najiandaa
kufaulu mtihani
wewe je?
GEOPHREY E. SANGA @2015 GEOPHREY E. SANGA 2015 GEOPHREY E. SANGA 2015 GEOPHREY E. SANGA
Kitabu hiki kinalenga kumsaidia mwanafunzi
kumwelekeza njia mbadala za usomaji na jinsi ya
kujiandaa na mtihani. Kitabu hiki kinamsaidia
mwanafunzi kujua namna ya kusoma namna na
kukabiliana na mtihani na namna ya kujibu maswali
ya mtihani.
Kupitia kitabu hiki mwanafunzi atajiamini wakati wa
mtihani na hivyo kupelekea ufaulu mkubwa.
GEOPHREY E. SANGA ni mwalimu wa
masomo ya sanaa na TEHAMA (ICT),
amehitimu shahada ya kwanza ya
elimu katika chuo kikuu cha Dodoma
(UDOM) (Bed –ICT)
Amehitimu kidato cha sita katika shule ya secondary
TUKUYU, kidato cha nne katika shule ya sekondari
IPANDE na alihitimu shule ya msingi NKOKWA
Kimepigwa chapa na
kabuje stationary @2015
Kyela-Mbeya- Tanzania
3. SHUKRANI
Shukrani zangu za pekee ziende kwa wenyezi mungu mwingi wa
rehema anayenijaalia afya njema na kunifanya niwe mzima ili
niendelee kuifanya kazi hii, na kunikarimu uwezo wa kiakiri na
maarifa katika kuandika kitabu hiki.
Pia shukrani zangu ziende kwa familia yangu (Mariamu Kabuje na
Jamaly Sanga) kwani wamenisaidia mchango wao wa hali na mali
na kunitia moyo katika uaandaaji wa kitabu hiki
Pia niwashukuru wale waliotoa mchango wao wa mawazo juu ya
kuandaa kitabu hiki. Wapo wengi sana ntawataja wachache tu,
nimshukuru Happiness George Tarimo mwalimu wa saikolojia,
Kiswahili na Geograph kwa mchango wake mkubwa
Mwisho niwashukuru walimu wangu wote wa walio nipa maarifa ya
kufika hapa nilipo. Shukrani kwa walimu wa shule ya msingi
nkokwa (1991-2005), walimu wa shule ya sekondari Ipande[o-level]
(2006-2009), walimu wa shule ya sekondari Tukuyu[A-level] (2010-
2012) pamoja na wahadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma (UDOM)
kitibo cha elimu (2012-2015)
4. UTANGULIZI
Kitabu hiki kimeandaliwa kwa lengo la kumsaidia mwanafunzi kufaulu mitihadi
yake vizuri. Kitabu hiki kitamwongoza mwanafunzi namna ya kusoma wakati wa
kujiandaa na mitihani. Kitamwongoza na kumpatia mwanafuzi njia au mbinu bora za
kujiaandaa na mitihani
Pia kitabu hiki kinampa mwanafunzi mbinu bora za kukabiliana na mtihani siku ya
mtihani na siku zote awapo kwenye mchakato wa ufanyaji mtihani.
Kitabu hiki hakikusahau pia kumweleza mwanafunzi uhusiano wake na jamii yake
yaani wazazi na walimu wake kwani nao wana mchango mkubwa katika ufaulu wa
mwanafunzi.
5. TABARUKU
Kitabu hiki nakitabaruku kwa Familia yangu ya Mariamu Kabuje kwani wao ni
tegemeo langu la pekee.
Mungu awape maisha marefu na mzidi kumtegemea yeye.
Kupitia kuandika kitabu hiki nimejifunza vitu vingi sana na sitaacha kuandika kama
mwenyezi mungu ataendelea kunipa afya na akili
“si rahisi kupaza sauti kutoka nyikani na ukapata msaada kwa haraka”
6. SURA YA KWANZA
UTANGULIZI.
Wanafunzi wengi wamekuwa wakijiuliza maswali mengi juu ya namna ambayo wanaweza kufauru
mitihani yao.
Wingi wamekua wakijua swala la kufauru mitihani ni swala la watu wachache (wenye akili), lakini
ukweli ni kwamba hakuna mtu mwenye akili na asiye na akili wala mwenye akili bali
tunatofautiana IQ (uwezo binafsi) . uwezo huu ndio unamfanya mtu kuelewa haraka ama
kuchelewa kuelewa ila mwisho wa siku wote tunaelewa kwa pamoja haijalishi unaelewa haraka au
umechelewa kuelewa lengo ni kuelewa.
Licha ya IQ kutofautiana wengine huwa na IQ kubwa lakini bado wanachelewa kuelewa kutokana
na mbinu wanazotumia kusoma. Kitabu hiki kitakupa mbinu mbalimbali zitakazo kuwezesha
wewe kama mwanafunzi kuweza kufauru mtihani wako haijalishi unasoma shule ya kata (wengine
huziita shule za kayumba) au unasoma shule za private kitabu hiki kitasaidia sana kufikia malengo
yako ya ufauru mkubwa sasa (big result now)
MASWALI 10 YA KUJIULIZA.
1. Mtihani ni nini?
2. Kwa nini kuna mitihani?
3. Anayetunga mtihani ni nani?
4. Kwa nini anatunga mitihani?
5. Maswali ya mtihani yanatoka wapi?
6. Kwanini tunafeli mitihani?
7. Mtihani unajibiwa ukiwa na hali ganii (mud)?
8. Ntafanyeje ili kuweza kufaulu mitihani yangu?
9. Nifanye vitu gani kabla ya kuingia kwenye chumba cha mtihani?
10. Ni kina nani wanaopaswa kufaulu mitihani?
Maswali haya na mengine mengi yatajibiwa ndani ya kitabu hiki ili kuweza kumtoa mwanafunzi
katika hali ya kujiuliza maswali mengi kuhusiana na mtihani ili kumsaidia kuukabili mtihani bila
kuwa na maswali mengi ya kujiuliza mwisho wa siku matokeo makubwa.
MAJIBU YA MASWALI
7. Maswali haya yatajibiwa kwa ufupi na kwaeleweka katika sehemu hii, yataendelea kujibiwa kwa
undani na kwa maelezo ya kina katika sehemu nyingine kadri utakavo edelea kusoma itabu hiki
utapata majibu ya ziada. Tuanze swali moja baada ya linguine.
1. Mtihani ni nini?
Mtihani ni jumla ya maswali yaliyoandaliwa kutoka kwenye mada alizosoma mwanafunzi darasani
kwa lengo la kumpima kama ameelewa ama hakuelewa kwenye mchakato wa ujifunzaji. Mtihani
uweza kufanyika mwanzoni mwa mchakato, katikati ama mwishoni mwa mchakato wa ujifunzaji
ili kumwamisha mwanafunzi kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine.
2. Kwa nini kuna mitihani?
Mitihani huwekwa ili kumpima mwanafunzi kama alielewa wakati wa mchakato wa ujifunzaji ili
kujua kitu gani alielewa ama hakuelewa sehemu gani au kumwamisha kutoka hatua moja ya
kielimu kwenda kwenye hatua nyingine ya juu zaidi. Wanafunzi wengi wanamini kuwa mitihani
hutungwa ili kupunguza idadi ya wasomi hivyo kuwafanya wakate tama ya kusoma.
3. Anayetunga mtihani ni nani?
Anayetunga mtihani ni mwalimu. Wanafunzi wengi huamini kuwa wanaotungamitihani ni watu
wenye malengo mabaya na wanafunzi ili kuwafelisha. wanasahau
kuwa anayetunga mtihani ni mwalimu mwenye uelewa wa soma
na maada husika.
4. Kwa nini anatunga mitihani?
Anatunga mitihani ili kuwapima wanafunzi wanaozingatia masomo na wasiozingatia masomo,
wanalio elewa na wasio elewa. Wanafunzi wengi huamini kuwa mwalimu hutunga mitihani ili
kumfelisha mwanafunzi, jambo lisilo kweli.
5. Maswali ya mtihani yanatoka wapi?
Maswali ya mtihani hutoka kwenye mada zilizofundishwa na mwalimu au mada zilizoainishwa
kwenye mtaala wa elimu na kupangiliwa kwenye muhtasari wa somo na si nje ya hapo. Hivyo
maswali hutoka kwenye vitabu
6. Kwanini tunafeli mitihani?
8. Wanafunzi wengi hufeli mitihani kutokana na kukosa mbinu bora za kusoma/kujiandaa na mtihani
na namna ya kujibu mtihani. Sio kila anayefeli hana akili bali alikosa mbinu za kujisomea na
kujibu mitihani.
7. Mtihani unajibiwa ukiwa na hali ganii (mud)?
Mtihani hujibiwa ukiwa katika hali ya kawaida ya kutokuwa na wasiwasi wala pressure yoyote.
Wanafunzi wengi huingia kwenye chumba cha mtihani wakiwa na wasiwasi mkubwa au pressure
kubwa ya kukabiliana na mtihani hivyo kuwapelekea kufeli mitihani.
8. Ntafanyeje ili kuweza kufaulu mitihani yangu?
Wanafunzi wengi wamekuwa wakijiuliza maswali mengi ya namna gani wanaweza kufahuru
mitihani yao. Wengi wamekuwa wakienda hadi kwa waganga wa kienyeji. Lakini mbinu pekee ni
kusoma na kuchagua mbunu sahihi za usomaji na ujibuji wa mitihani.
9. Nifanye vitu gani kabla ya kuingia kwenye chumba cha mtihani?
Kitu cha kwanza ni kujiandaa vya kutosha kabla ya siku ya mtihani kuhakikisha kila kitu
umekipitia na kukielewa kwa kutumia mbinu bora za usomaji na wakati wa mtihani hakikisha
unatoa wasiwasi wote kwa kujiamini kama unaweza, na mwisho kutumia mbinu bora za kuchagua
maswali na kujibu maswali.
10. Ni kina nani wanaopaswa kufaulu mitihani?
Wanafunzi wengi huona wanaopaswa kufaulu mitihani ni watu Fulani, kumbe kila mwanafunzi
ana uwezo wa kufaulu mtihani haijalishi anaelewa halaka au anaelewa taratibu.
Baada ya kukabiliana na maswali mengi yanayo wasumbua wanafunzi wengi sasa najua
wanafunzi wengi watakuwa na uelewa juu ya mtihani. Hivyo mwanafunzi anapoenda kuzitumia
mbinu za kufauru mtihani atajitambua yeye ni nani na mtihani ni nini hivyo kumfanya awe tayari
kuzitumia mbinu tutakazozieleza hapo mbele.
9. SURA YA PILI
MBINU ZA KUJIANDAA NA MTIHANI KABLA YA MTIHANI
1: kuhuzuria vipindi vyote vya darasani.
2: Kuchukua/ kuandika mambo muhimu wakati wa kipindi.
3: kuandika nukuu (notes) zote unazopewa na mwalimu
4: kutafuta nukuu (notes) nyingine mbali na za mwalimu
5: kusoma material zote ulizonazo
6: kupitia mitihani ya nyuma kutafuta past paper
1: kuhuzuria vipindi vyote vya darasani.
Wanafunzi wengi wamekuwa wavivvu wa kuhuzuria vipindi vya
darasani na badalaa yake kutumia nguvu zao kusoma kile
kilichofundishwa na mwalimu darasani. Na hakikisha unashiriki
kujibu na kuliza maswali darasani ili uelewe zaidi
Kuna umuhimu gani mwanafunzi kuhuzuria darasani?
Kwanza itakusaidia kukumbuka maelezo ya point muhimu hivyo kukusaidia wakati wa
kusoma kutotumia nguvu nyingi kuelewa.
Humsaidia mwanafunzi kunukuu point muhimu wakati mwalimu anafundisha
Humsaidia kujua ni mambo gani anapaswa kuyafahamu kwenye mada husika hivyo
kumpunguzia mzigo wa kusoma mambo mengi yasiyo na umuhimu (yaliyo nje ya
muhtasali wa somo) kwani mwalimu atakupa mwongozo wa mambo unayotakiwa kusoma
Itakusaidia kuchambua mambo uliyokuwa uana uelewa nayo awali kama ulikuwa sahihi au
la na kama hukuwa sahihi kubadilisha na kuingiza jambo jipya unalopewa na mwalimu.
Namna ya kuandika nukuu (notes) darasani.
Wakati wa kuandika notes mwalimu akiwa anafundisha huitaji umakini mkubwa. Sio kila
mwalimu anachoandika ubaoni lazima uandike mengine huyandika ili kumsaidia kuelezea point ili
aeleweke. Hivyo unavyo kuwa unandika notes wakati mwalimu anafundisha zingatia yale mambo
10. mhimu hasa yale yanayotiliwa mkazo na mwalimu. Na kuwa makini kusikiliza maelezo kuliko
kukazania kuandika tu.
Andika pointi, maelezo kidogo, mfano. Maelezo mengine utasikiliza tu na kuyaweka kichwani.
2: Kuchukua/ kuandika mambo muhimu wakati wa kipindi.
Mwanafunzi unatakiwa kuwa na daftari ndogo ambayo itakusaidia
kuandikia pointi muhimu wakati wa kipindi. Kwenye hilo daftari
utandika summary na sio notes hivyo utandika point tu. Zitakusaidia
wakati wa usomaji ili ujikite zaidi kwenye mambo muhimu pia
itakusaidika kutosinzia wakati wa kipindi
3: kuandika nukuu (notes) zote unazopewa na mwalimu.
Mwanafunzi unatakiwa kuandika nukuu zote unazopewa na mwalimu kabla,
baada na wakati wa kipindi. Kuna baadhi ya walimu hupenda kutoa notes
kabla ya kipindi wenginee baada na wengine wakati wa kipindi hivyo uwe
makini kuzipata notes zote maana ndizo zitakuwa mwongozo wako wakati
wa usomaji. Usipendelee kuandika notes kutoka kwa mwanafunzi
mwenzako maana unaweza ukakopi makisa aliyo andika yeye ni vyema
kuandika nukuu mwenyewe kutoka kwa mwalimu.
4: kutafuta nukuu (notes) nyingine mbali na za mwalimu
Mwanafunzi unatakiwa kufanya jitihada kubwa ya kutafuta notes
nyingine mbali na zile ulizopewa na mwalimu ili kuongeza ujuzi
zaidi. Nukuu hizo unaweza kuzipata kwenye mtandao, vitabu vya
kiada na ziada, vitini nk.
5: kupitia mitihani ya nyuma kutafuta past paper
Mwanafunzi inakubidi uwe na jitihada ya kutafuta mitihani ya nyuma, mitihani hii tafuta ya
shuleni kwenu, shule nyingine na mitihani ya mocko na mitihani ya taifa hii itakusaidia wakati wa
usomaji. Tutangalia kwenye point ya sita namna ya kusoma kwa kutumia mitihani ya nyuma.
5: kusoma material zote ulizonazo
Njiia za usomaji.
Kuna njia nyingi zitumikazo katika usomaji lakini tutangalia njia tatu muhimu.
11. Kusoma pekeyako (individual studies)
Kusoma kwenye vikundi (group discussion)
Kusoma kwa kuliza maswali
Kusoma pekeyako (individual studies)
Katika jia ya kusoma pekeyako, mwanafunzi unakaa pekeyako
kwenye meza na kusoma. Katika usomaji huu mwanafunzi unaweza
ukawa unatumia notes kusoma, au maswali yaliyomo kwenya past
paper au sehemu yoyote.
Namna ya kusoma notes. Wanafunzi wengi wamekuwa wakisoma notes kama wasomavyo vitabu
vya hadithi au gazeti na kuwapelekea kusinzia haraka au kuto kuelewa.
Unaposoma notes epuka kukalili soma na uelewe points hii itakua rahisi kwa wewe kukumbuka
kwa ulahisi points na maelezo yake. Na unapo soma note kumbuka kuwa na karatasi au daftari la
lafu kila unapo maliza kusoma sehemu unarudia kwa kuandika point zote ulizozisoma kama
unazikumbuka usihame kama bado hukuzishika vizuri rudia tena kusoma.
Pia unaweza kutumia maswali ya mada husika kusoma notes ili yakuongoze katika kusoma au
kujua maeneo unayotakiwa kutilia mkazo katika usomaji wako ( unaweza kutumia maswali ya past
paper au yaliyomo kwenye vitabu vya kiada au vya zaiada.)
Kusoma maswali. unapo soma maswali kumbuka kuwa na nukuu zote ili kupitia pale ambapo
unakuwa umeshindwa kujibu swali. Hapa pia unatakiwa kuwa na karatasi utakalo tumia kuandika
point au kusolvia swali lako. Na kama umesahau point au kanuni ya kufanya swali lako unarejea
kwenye nukuu zako. Au uatajibu maswali yote na baadaye kurejea kwenye notes zako kama
ulikuwa sahihi au hukuwa sahihi na kama hukuwa sahihi unajifanyia usahihi.
Kusoma kwenye vikundi (group discussion)
Hapa unavyotengeneza vikundi vya kujisomea hakikisha unalia
watu mnaoendana mwenendo na itikadi na mwenendo yenu na
usawa wa masomo yenu sciences au arts.
Mnapo fanya discussion mnaweza kutumia maswali au kupitia
notes na kuelekezana maeneo ambayo hayakueleweka darasani
Kuwa huru kuuliza swali lolote pasipo kuogopa maana unakuwa upon a wanafunzi wenzako hivyo
ni lahisi kuwauliza maswali.
12. Hakikisha unachangia mawazo ili kutoa kile ulicho nacho na unapo waelekeza wenzako inakuwa
rahisi wewe kuhifadhi zaidi kichwani
Usisahau kuandika opoint mnazofikia mwafaka kuwa ni sahihi.
Epuka kuingiza maada zilizo nje na somo, kwani wanafunzi wengi hujikuta wakiongelea mambo
yaliyonje na somo na kutumia mda mwingi kulijadili na kutumia mda mchache kujadili vitu vya
msingi.
Hakikisha unakuwa naratiba ya discussion ili upitie
kwanza yale mtakayoenda kujadili na wenzio ili usije
ukaenda ukiwa mtupu na ukashindwa kuchangia.
Baada ya discussion tenga mda wa kuyapitia yote mlio
jadili. Na sehemu ambazo hamkufikia mwafaka ni vema
mkamwona mwalimu wa somo au kikundi kingine cha
wanafunzi wenzenu au mwanafunzi mmoja mwenye
uelewa na sehemu hiyo.
Na ni vyema mkajiwekea utaratibu wa kutungiana mitihani angalau mara moja kwa wiki.
Mtapeana zamu ya kutunga mtihani ili kujipima kama mnayo jadiliana mnaelewa na kama hiyo
haitoshi mnaweza kumwomba mwalimu akawatungia maswali na mtafanya kwa uaminifu kwa
kujisimamia wenyewe na kumrudishia mwalimu awasahihishe.
Kusoma kwa kuliza maswali
Hapa unaweza kuwa unandaa maswali angalau matano kila
siku unayoona yamekushinda na ukampelekea mwalimu wa
somo husika au mwanafunzi mwenzako. Unapokuwa
unaelekezwa ndivyo utajifunza zaidi.
Nb: jitahidi kutumia njia zote wakati wa kusoma, usije ukatumia njia moja tu ya kusoma mfano
kusoma peke yako muda wote au mda wote kwenye group kufanya discussion bila kuwa na mda
wako binafsi wa kupitia mliyo discussi na uliyosoma darasani au kuliza maswali tu. Tenga mda
wako kusoma pekeyako mda mwingine kwenye discussion na kuliza maswali hivyohivyo kuwa
na ratiba inayoeleweka na hakikisha unaifuata vyema ratiba yako.
13. SURA YA TATU
NAMNA YA KUJIBU MASWALI WAKATI WA MTIHANI
Baada ya kujiandaa kwa muda mrefu sasa unatakiwa kuyawasilisha yaleyote uliyosoma kwa muda
mfupi sana masaa mawili au matatu. Hapa ndipo wanafunzi weengi huingiwa na wasiwasi
mkubwa sana.
Kabla ya kuingia kwenye chumba cha mtihani
Kabla hujaenda kwenye chumba cha mtihani hakikisha unajikagua na kuhakikisha
una vifaa vyote vinavyorhusiwa kwenye chumba cha mtihani. Hii itakusaidia
kuwa huru kwenye mtihani pasipo kumsubiria mwenzako amalize kufanya swali
ndipo uazime, hiyo itakuharibia mudi ya kufanya mtihani na kwangukia katika
kufeli
Hakikisha huungii na kitu kisichoruhusiwa kuingia nacho kwenye chumba cha
mtihani maana ukiingia nacho kitakufanya uwe na wasiwasi mkubwa kukamatwa
na unajikuta unashindwa kufanya mtihani wako kwa uhuru.
Ni vyema kuingia na saa kwenye chumba cha mtihani hii itakusaidia kutenga
mda wako ili ujue swali moja utatumia dakika ngapi ili ukamilishe maswali
yako kwa wakati na ukijiona uko nje ya mda uongeze speed ya kuandika,
kuliko kusubiria msimamizi aseme wengine huwa wanajisahau kusema
utasikia bado dk 10 wakati wewe bado hujafanya maswali mengi hiyo nayo
siyo njeme.
Baada ya kuingia kwenye chumba cha mtihani
Unapofika na kukaa kwenyekiti jitahidi kusali kwa imani yako (imani huponya)
Baada ya kukabidhiwa karatasi relax kuwa huru usiwe na pressure chukulia ni sawa na test au
maswali uliyowahi kufanya darasani au sehemu yoyote ile.
Usifunue karatasi hadi pale utambiwa funua karatasi na msimamizi. Unaweza ukachungulia
mtihani afu ukakutana na swali gumu likakutia pressure na ukauona mtihani wote ni mgumu.
Andika taarifa zako za msingi (no ya mtihani au jina kama linahitajika) kabla hujaingia kuagalia
mtihani
14. Baada ya kuambiwa fungua mtihani soma kwanza maelekezo ya juu kabla ya kusoma maswali.
Baada ya kumaliza kusoma maelekezo ya mtihani kagua karatasi yako kama ina idadi sawa za
kurasa kama ulivo kwisha kuelezwa kwenye maelekezo, kagua idadi ya sehemu kama mtuhani
umegawanyika katika sehemu, pia kagua idadi ya maswali kama yako sawa na maelezo ya juu.
Usisahau kukagua aina ya mtihani kama ni civics hakikisha umepewa mtihani wa civics na kama
ni form II hivyo hivyo.
Baada ya kufanya hivyo tulia kwa muda wa sekunde kadhaa vuta pumzi hadi mwili ukae katika
usawa.
Sasa anza kusoma swali moja baada ya jingine soma kwa umakini swali zima sio kusoma maswali
nusu nusu. Soma maswali yote rudia mara mbili a tatu na uyaelewe maswali vizuri.
Baada ya kusoma maswali yako angalia swali lililo lahisi zaidi dilo uanze nalo. na unavyo anza
tena kujibu angalia swali hilo uliloanza nalo lipo sehemu gani na soma kwa umakini maelezo ya
sehemu hiyo. Faida ya kuanza na swali jepesi linakupa mwanga wa kujibu maswali mengine na
linakupunguzia pressure ya mtihani ili unapo fuata maswali magumu unakuwa huna pressure tena
ya mtihani.
Na unapochagua swali hakikisha umeandika point pembeni (mwishoni mwa kitabu cha kujibia
mtihani) ukiona unakumbuka point chache chagua linguine na kama ni hesabu hakikisha unandika
kanuni na unaikumbuka vizuri ndipo uanze kujibu na kama hukumbuki vizuri kanuni anza na
linguine ili pressure ikipungua utakumbuka vizuri kanuni.
Na unapo jibu swali hakikisha unangalia idadi ya alama katika swali unalo fanya usije ukatumia
muda mwingi kwenye swali la alama chache. Swali la alama chache maanake ulijibu kwa ufupi na
kwa kueleweka.
Epuka kumsumbua mau kusumbuliwa na mtu kwenye chumba cha mtihani. Mfano mwenzako
anakuomba umsaidie swali la kumi wakati wewe umelifanya mda, unaanza kurudi nyuma
kumwonyesha, kwanza unapoteza mda wako, pili mtiririko wako wa kujibu swali ulilokua unajibu
kwa wakati huo hupotea tatu unaingiza pressure tena kwa kuogopwa kukutwa na msimamizi hivyo
kupoteza umakini wa kujibu maswali.
Epuka kuangalia kwa mwenzako, maana mwenzako anaweza akawa amekosa na ukajiona wewe
ndo umekosa na kukata jibu lako sahihi na ukandika la mwenzako la uongo au lisilo sahihi.
15. Epuka kutoka toka nje wakata wa mtihani na kujikuta unatumia mda mwingi nje badala ya kujibu
maswala labda kama hali yako ya kiafya sio nzuri na kama upo fizuri mambo yote maliza kabla ya
kuingia kwenye mtihani.
Hakikisha unandika namba ya swali katika kila ukurasa wa karatisi yako
Baada ya kumaliza kufanya maswali yako hakikisha umejibu maswali yote ulio ambiwa ujibu.
Kuwa makini sana na maswali ya lazima.
Kama umejiona umekamilisha maswali yote, sasa kagua namba za maswali katika kila ukurasa na
kisha kagua taarifa zako kama uliandika katika kila ukurasa wa kitabu cha kujibia mtihani.
Unapotoka kwenye chumba cha mtihani epuka kusimuliana ya kwenye mtihani. Maana unaweza
ukambiwa umekosa swali ikakuharibia hata katika mtihani mwingine. Mambo ya mtihani yaishie
kwenye chumba cha mtihani.
NB: hakikisha kipindi chote cha mitihani unakuwa na ratiba ya mtihani inayokuongoza ni somo
gani linaanza na lipi linafuata, ili usije changanya ratiba.
Na kwa kipindi chote cha mtihani epuka kukaa peke yako, usije ukasinzia na ukapitiliza mda wa
mtihani, pia ukikaa peke yako hata ukikosea kunakili ratiba hakuna atakaye kurekebisha. Hivyo si
vyema kukaa peke yako kipindi chote cha mti
Kwa kusoma kitabu hiki najua utajifunza kitu na ukiyazingatia yote kufeli mtihani
kwako itakuwa si rahisi.
MWISHO